Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Dar: Maji yamenifika shingoni
Habari za Siasa

Meya Dar: Maji yamenifika shingoni

Spread the love

ISAYA Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam anaonekana kukata tamaaa, ni baada ya kuundiwa kamati ya kuchunguza kuhusu tuhuma zinazomkabili. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Akizungumza na kituo cha Redio cha East Africa mtandaoni leo tarehe 6 Januari 2019, Mwita ameeleza, haoni mwanga mbele bali giza nene, na kwamba kilichobaki ni kumwachia Mungu.

Mwita anatuhumiwa kutotumia Sh5.8 bilioni za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), matumizi mabaya ya gari ya ofisi, kushindwa kuongoza kikao cha baraza la madiwani pia kupendelea baadhi ya mameya kuingia katika kamati za fedha.

Amesema, tuhuma anazobebeshwa nazo na hata kusababisha Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuunda kamati ya kumchunguza, hazina ukweli wowote.

“Kiukweli sasa maji kwangu yapo shingoni, mbele sioni wala nyuma sioni ila naamini Mwenyezi Mungu atasimama,” amesema Mwita.

Akizungumzia kisa cha kubebeshwa tuhuma hizo Mwita amedai, tatizo lilianzia kwenye matumizi ya pesa za UDA, “pesa hizo hatukuzitumia kutokana na malalamiko ya baadhi ya wananchi, sasa nimeshangaa ambao tulikubaliana kutozitumia wananilalamikia mimi,” amesema.

Kuhusu tuhuma za matumizi mabaya ya gari la ofisi, Isaya amesema, dereva wake alisababisha ajali katika eneo la Ubungo na kwamba kwa kuwa wanamsakama, wameshikilia suala hilo kuwa matumizi mabaya ya gari hilo.

“Dereva wangu alisababisha ajali katika eneo la Ubungo, kwa hiyo madiwani wamelalalamikia mimi nimetumia chombo cha moto vibaya, yaani wamenikalia kooni kweli,” amesema na kuongeza;

“Umeya wangu sasa unapimwa ikiwa imebaki miezi mitatu kabla hatujavunja Baraza la Madiwani, na hivi karibuni nimeanza kupata wakati mgumu kwenye kiti changu, naomba masheikh na viongozi wengine wa dini waniombee.”

Mwita ambaye ni diwani wa Vijibweni (Chadema) na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, aliyechaguliwa mwaka 2016.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!