FAINALI ya michuano ya Copa America, itapigwa siku ya Jumapili ambapo itaikutanisha miamba ya soka barani humo, tumu ya Taifa ya Argentina dhidi ya Brazil. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Mchezo huo ambao utapigwa siku ya Jumapili, utakwenda kushuhudia mastaa wawili wa timu hizo, Lionel Mess, pamoja na Neymar Do Santos, wakipigania kutwaa taji hilo, ambao walicheza pamoja ndani ya klabu ya FC Barcelona.
Wachezaji hao wawili walicheza kwa pamoja misimu mine kuanzia 2013/17, wakiwa ndani ya kikosi cha Barcelona na kuchukua jumla ya mataji saba na baadae Neymal kuamua kutimkia Psg ya Ufaransa.
Argentina inaongozwa na Messi imetinga fainali mara baada ya kuiondosha Colombia, kwenye hatua ya nusu fainali kwa mikwaju ya penati 3-2, mara baada ya kumaliza dakika 90, wakitoka sare ya bao 1-1.
Kwa upande wa Brazil walitinga hatua ya fainali mara baada ya kuifunga timu ya Taifa ya Peru, kwa bao 1-0.
Katika michuano hiyo lionel Messi ndio kinara kwa ufungaji, akiwa na mabao manne, na Neymal akishika nafasi ya tano kwenye idadi ya wafungaji wa michuano hiyo, akiwa na mabao 2.
Leave a comment