Mshambuliaji wa mpya wa klabu ya PSG Raia wa Argentina Lionel Messi amefungua rasmi akauti ya mabao katika klabu yake hiyo, mara baada ya jana kupachika bao moja kwenye ushindi waliopata wa mabao 2-0, kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Manchester City. Damas Ndelema TUDARCo….. (endelea)
Mchezo huo wa kundi A Ulipigwa jana kwenye dimba la Parc Des Princes na wenyeji Psg kufanikiwa kuondoka na pointi tatu.
Mchezaji huyo hakua na mwanzo mzuri katika klabu yake hiyo mpya kama wengi walivyotarajia baada ya kucheza michezo kadhaa bila kushinda tofauti na mpinzani wake mkubwa Cristiano Ronaldo ambaye alikua na mwanzo mzuri katika klabu yake mpya ya Manchester United.
Messi ilimlazimu kusubiri mpaka siku ya jana na kufunga goli hilo katika mchezo wa Ligi ya mabigwa barani Ulaya dhidi ya Manchester City ambapo goli la kwanza la uongozi likifugwa na mchezaji Idrissa Gueye ‘’Gana’’
Pia michuano hiyo iliendelea kwa kupigwa mechi mbalimbali baada ya kushuhudia Liver pool wakiubuka na ushindi mnono ugenii wa mabao 5-1 dhidi ya FC porto ya nchini ureno , huku mabigwa mara kumi na tatu wa michuano hii ya klabu bigwa barani Ulaya timu ya Real Madrid wakikubaki kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Sheriff Fc ya nchini Moldovia na kufanya waongoze kundi wakiwa na jumla ya pointi sita , pia Ac milan walichoshana nguvu na Atletico Madridi kwa kutoka sare ya bao1-1, Dortmund 1 Vs 0 Sporting cp , Leipzing1 Vs Club Brugge , shakhtar Donestk 0 Vs 0 Inter Milan
Leave a comment