Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Messi afungua akauti ya mabao PSG
Michezo

Messi afungua akauti ya mabao PSG

Spread the love

 

Mshambuliaji wa mpya wa klabu ya PSG Raia wa Argentina Lionel Messi amefungua rasmi akauti ya mabao katika klabu yake hiyo, mara baada ya jana kupachika bao moja kwenye ushindi waliopata wa mabao 2-0, kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Manchester City. Damas Ndelema TUDARCo….. (endelea)

Mchezo huo wa kundi A Ulipigwa jana kwenye dimba la Parc Des Princes na wenyeji Psg kufanikiwa kuondoka na pointi tatu.

Mchezaji huyo hakua na mwanzo mzuri katika klabu yake hiyo mpya kama wengi walivyotarajia baada ya kucheza michezo kadhaa bila kushinda tofauti na mpinzani wake mkubwa Cristiano Ronaldo ambaye alikua na mwanzo mzuri katika klabu yake mpya ya Manchester United.

Messi ilimlazimu kusubiri mpaka siku ya jana na kufunga goli hilo katika mchezo wa Ligi ya mabigwa barani Ulaya  dhidi ya Manchester City ambapo goli la kwanza la uongozi likifugwa na mchezaji  Idrissa Gueye ‘’Gana’’

Pia michuano hiyo iliendelea kwa kupigwa mechi mbalimbali baada ya kushuhudia Liver pool wakiubuka na ushindi mnono ugenii wa  mabao 5-1 dhidi ya FC porto ya nchini ureno , huku mabigwa mara kumi na tatu wa michuano hii ya klabu bigwa barani Ulaya timu ya Real Madrid wakikubaki kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Sheriff Fc ya nchini Moldovia na kufanya waongoze kundi wakiwa na jumla ya pointi sita , pia Ac milan walichoshana nguvu na Atletico Madridi kwa kutoka sare ya bao1-1, Dortmund 1 Vs 0 Sporting cp , Leipzing1 Vs Club Brugge , shakhtar Donestk 0 Vs 0  Inter Milan

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!