KUONDOLEA kwa Mwigulu Nchemba katika nafasi ya Waziri wa Mambo na Ndani ya Nchi kumezua mijadala mikali kwa wadau wa siasa, huku kila mmoja akitoa sababu za kuondolewa kwake katika nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Mwigulu aliondolewa katika nafasi ya uwaziri baada ya Rais John Magufuli kufanya marekebisho madogo katika baraza la mawaziri na nafasi yake kuchukuliwa na Kange Lugola.
Baada ya Mwigulu kuondolewa wadau wa siasa wamegawanyika katika pande mbili, huku kila upande ukielezea sababu za kuondolewa kwake.
Upo upande unaoamini kuwa Mwigulu ameondolewa kwa kwenda tofauti na mfumo wa Serikali ya Awamu ya Tano, lakini wengine wakiamini kuwa ametumbuliwa kutokana na kushindwa kusimamia majukumu yake katika nafasi aliyokuwa nayo kama Waziri wa Mambo ya Ndani.
Baadhi ya maoni ya wadau hao katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kuondolewa kwa Mwigulu.
Cde Karibu Sana! Tuliolelewa humu ni kama Mwanzi, upepo ukivuma Mwanzi unalala, upepo ukiisha Mwanzi unasimama ukiwa imara zaidi! Tuwatumikie waliotupa kura! pic.twitter.com/6mUcEwsPwm
— Nape Moses Nnauye (@Nnauye_Nape) July 1, 2018
Allen mimi najua kuwa Mwigulu hahusiki na watu waliopetezwa. Najua Mwigulu aliagiza uchunguzi wa matukio kadhaa ya utekaji na hata mauaji na alikwama sababu chombo kinachofanya hayo hakikuwa kwake. Mimi Kama Kiongozi naona mbali, najua kuondolewa Mwigulu hakuhusiani hayo. https://t.co/RyAHGa362V
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) July 1, 2018
Mh Mwigulu,Mungu anakupenda sana ukitafakari utapaswa kumshukuru.
Mh Kange umekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nakuombea kwa Mungu ujue kuwa Binadamu ni Roho anayo Nafsi anaishi katika Mwili.Angalia mwili wako na akili zako zisiangamize Roho yako katika wajibu huu mgumu.— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) July 1, 2018
https://twitter.com/Julius_Mtatiro/status/1013415733424984064
Nani aliyewaambia kuwa kaondolewa kisa waraka wa KKKT? Ache ni kuhadaa watu. Mwigulu aliwahi kunaswa vibao na Magufuli pale Ikulu, yet hakujiuzulu. Huyu wa kumpongeza kwa kutimuliwa? Come one guys, jaribuni kuficha unafiki wenu. Please! https://t.co/7ssQbfGtpn
— 𝐉𝐚𝐬𝐮𝐬𝐢 (@Chahali) July 1, 2018
Leave a comment