Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe ambwaga Cyprian Musiba, kulipwa bilioni 6
Habari za SiasaTangulizi

Membe ambwaga Cyprian Musiba, kulipwa bilioni 6

Mmiliki wa Gazeti la Tanzanite, Cyprian Musib
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imemuamuru Mmiliki wa Gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba kumlipa aliyekuwa Waziri mambo ya nje, Bernard Membe kiasi cha Sh. 6 bilioni kama fidia ya kumchafua kupitia vyombo vyake vya habari. Anaripoti Ulwe R. Ulwe, Dar es Salaam … (endelea)

Hukumu hiyo ya shauri la kesi namba 220 ya mwaka 2018, imetolewa leo tarehe 28 Oktoba, 2021 na Jaji Joacquine De Mello.

Amesema pamoja na Musiba kutakiwa kumlipa Membe Sh bilioni sita, pia ametakiwa kulipia gharama za kesi hiyo.

Amesema hukumu hiyo pia inatoa zuio la kudumu la kutomkashifu Membe au kusema uongo dhidi yake na kulipa gharama za kesi.

Amesema katika kiasi hicho cha Sh bilioni sita, Sh bilioni tano ni fidia ya hasara halisi na Sh. bilioni moja hasara ya jumla.

Katika kesi hiyo Membe alimshtaki Musiba, Mhariri wa gazeti la Tanzanite na wachapishaji wa gazeti hilo ambapo aliwadai Sh. bilioni 10.3 kwa kumchafua.

Musiba katika kesi hiyo alishtakiwa kwa kumtuhumu Membe kuwa anamhujumu Rais John Magufuli (wakati huo) asitekeleze majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Pia alidai kwamba mbinu mojawapo ya kukamilisha hujuma hizo ni maandalizi aliyokuwa akifanya ya kugombea urais mwaka 2020 kupitia CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!