Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdude wa Chadema huru, shangwe zarindima mahakamani
Habari za SiasaTangulizi

Mdude wa Chadema huru, shangwe zarindima mahakamani

Mdude Nyagali (katikati) akiwa mahakamani muda mchache kabla ya kuachiwa huru
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Mbeya imemwacha huru, Mdude Nyangali maarufu ‘Mdude Chadema,’ baada ya Jamhuri kushindwa kuthibitisha madai yake kuhusu kusafirisha dawa za kulevya katika kesi ya Jinai Na. 36/2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya…(endelea).

Zawadi Laizer, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, ametoa hukumu hiyo leo tarehe 28 Juni 2021, mkoani humo.

Hakimu Laizer ameeleza kuwepo kwa mashaka ya kuwapo kwa uwezekano kuwa, dawa za kulevya ziliwekwa na polisi nyumbani kwa Mdude ama wakati wa upekuzi au kabla ya upekuzi kufanyika.

Katika maelezo yake, hakimu huyo ameeleza, upekuzi nyumbani kwa Mdude ulikuwa batili kwa kuwa, ulifanywa kinyume cha utaratibu na sheria.

Akieleza hukumu hiyo, Hakimu Laizer amesema, funguo za mshatakiwa huyo, zilikuwa polisi na hazikuchukuliwa kwa namna sheria inavyoelekeza.

Wafuasi wa Chadema waliohudhuria kesi ya Mdude

Mdude amekaa rumande kwa siku 414 – mwaka mmoja na mwezi mmoja – tangu alipokamatwa Mei 2020 kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin, zenye uzito wa gramu 23.4.

Mdude alikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, tarehe 10 Mei 2020, baada ya kufanyiwa upekuzi katika hoteli moja jijini humo, alikokuwa amepanga ambapo alidaiwa kukutwa na dawa hizo.

Hukumu hiyo imetolewa leo baada ya kuahirishwa Jumatatu ya tarehe 14 Juni 2021, kwa kile kilichoelezwa na hakimu sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake.

Nje ya viunga vya mahakama, mara baada ya kuachiwa kwa Mdude, shangwe za wafuasi wa Chaadema zilitawala wakati wakitoka mahakamani wakiwa na ‘mtu wao’ Mdude ambaye waliombeba juu juu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!