Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee, wenzake 18 kufunguka
Habari za Siasa

Mdee, wenzake 18 kufunguka

Halima Mdee, Mbunge wa Chadema Viti Maalim
Spread the love

SIKU moja baada ya Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania, kuwafukuza uanachama, Halima Mdee na wenzake 18 kwa tuhuma za usaliti, wabunge hao wa viti maalum, watazungumza na waandishi wa habari kesho Jumapili 29 Novemba 2020 jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mdee na wenzake 18, walifukuzwa jana usiku Ijumaa, baada ya kikao cha siku nzima kufanyika chini ya Mwenyekiti, Freeman Mbowe jijini Dar es Salaam kuazimia kwa kauli moja wafukuzwe.

Mdee na wenzake, walikuwa wakituhumiwa kwa “usaliti, kughushi na uasi” wa chama hicho kwa kujipeleka kuapishwa tarehe 24 Novemba 2020 na Spika Job Ndugai kuwa wabunge wa viti maalum, wakijua chama hicho, hakijapendekeza majina yao Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Wabunge wengine waliofukuzwa ni wale waliokuwa wajumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Ester Bulaya na Esther Matiko. Katibu Mkuu wa Bavicha, Nusrat Hanje. Katibu Mkuu Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Grace Tendega.

Makamu Mwenyekiti Bawacha (Bara), Hawa Mwaifunga. Naibu Katibu Mkuu Bawacha, Jesca Kishoa na Katibu Mwenezi Bawacha, Agnesta Lambat.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa Mtwara, Tunza Malapo, Ceciia Pareso, Asia Mwadin Mohamed, Felister Njau, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Stella Siyao.Salome Makamba, Anatropia Theonest na Conchesta Lwamlaza.

Mbowe aliyetoa maazimio ya kikao hicho alisema, Mdee na wenzake 18, wanaweza kukata rufaa ndani ya siku 30 kwa Baraza Kuu la Chadema au kuomba radhi hadharani kwa walichokifanya.

Leo Jumamosi, MwanaHALISI Online, limezungumza na baadhi ya wabunge hao wa viti maalum kujua msimamo wao mpaka sasa ni upi mmoja wao amesema, “kwa sasa siwezi kusema lolote, tunamzungumzaji mmoja na atazungumza katika mkutano na waandishi wa habari.”

Mwingine ambaye alikuwa mjumbe wa kamati kuu amesema, “kesho tutazungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam. Karibuni na ninyi kwenye mkutano wetu. Mtaelezwe baadaye utakapofanyikia.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!