Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee, Matiko walivyomzungumzia Hayati Magufuli
Habari za Siasa

Mdee, Matiko walivyomzungumzia Hayati Magufuli

Spread the love

 

WABUNGE viti maalumu, Halima Mdee na Esther Matiko wamemchambua aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dk. John Magufuli (61), wakisema alikuwa kiongozi wa maendeleo ya vitu hasa miundombinu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato … (endelea).

Wanasiasa hao wametoa kauli hiyo jana Ijumaa tarehe 26 Machi 2021, Chato mkoani Geita, walikokwenda kuhudhulia maziko ya Hayati Magufuli.

Dk. Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya maradhi ya moyo.

Mdee alisema Dk. Magufuli ameacha alama katika sekta ya miundombinu, tangu alipokuwa waziri wa ujenzi hadi Rais wa Tanzania.

Nimekuwa mbunge kwa muda na tulikuwa wabunge pamoja akiwa waziri wa ujenzi. Kitu kikubwa nitakachokumbuka amecha alama kwenye masuala mazima ya miundombinu,” alisema Mdee

“Alikuwa waziri wa ujenzi katika serikali ya Hayati Rais Benjamini Mkapa na Jakaya Kikwete na yeye amekuja kuwa rais, alama kubwa aliyoiacha ni miundombinu kwa mantiki ya barabara, madaraja, vivuko,” alisema Mdee.

Akizungumzia msiba wa Dk. Magufuli, Mdee alisema alishtushwa na kifo chake, kilichotangazwa tarehe 17 Machi 2021 na aliyekuwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan ambaye kwa sasa ndiye Rais.

“Nilipokea msiba wa Magufuli nikiwa Dodoma kamati za Bunge zinaendelea, nilipokea kwa mshtuko kama walivyopokea wengine sababu msiba unashtua,” alisema Mdee

Kwa upande wake Matiko alisema, miradi aliyoiacha Dk. Magufuli itasaidia kuondoa changamoto za nchi.

Aliitaja miradi hiyo ni, ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), madaraja, barabara, Bwawa kubwa la uzalishaji umeme (Sitigler’s Gorge), mradi wa kusambaza umeme vijijini (REA).

“Ni mtu ambaye alikuwa anahakikisha Tanzania inaboreshwa katika miundombinu, alijikita sana kwenye maendeleo ya vitu, barabara za kuunganisha mikoa na majimbo.”

“Lami alijitahidi kuweka, alijenga madaraja, SGR, bwawa la umeme ametumia trilioni za hela lakini ukikamilika utatua tatizo la umeme,” alisema Matiko.

Matiko alisema “kupitia mradi wa REA ameleta umeme vijijini. Katika miaka mitano ameweza kuondoa changamoto ya umeme kweye vijiji.”

Mbali na ujenzi wa miundombinu, Matiko alisema Dk. Magufuli ameacha alama ya sera ya elimu bure, ujenzi wa miradi ya maji na hospitali.

Vilevile, Matiko alisema Dk. Magufuli katika uongozi wake alifanikiwa kurudisha nidhamu kwa watumishi wa umma.

Dk. Magufuli alifariki dunia akiwa madarakani, akitumikia muhula wake wa mwisho wa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, aliyoutumikia kuanzia tarehe 5 Novemba 2020 hadi 17 Machi 2021, baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Muonekano wa kaburi la Hayati John Magufuli

Mwanasiasa huyo aliiongoza Tanzania kwa miaka zaidi ya mitano mfululizo, tangu alipoingia madarakani kwa mara ya kwanza tarehe 5 Novemba 2015.

Mwili wake umezikwa jana Ijumaa nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!