Friday , 2 June 2023
Habari za Siasa

Mdee atoka mahabusu

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera, limemwacha kwa dhamana Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Halima Mdee. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Jeshi hilo lilimshikilia Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, tangu jana tarehe 14 Julai 2019, kwa tuhuma za kufanya uchochezi.

Mdee, Grace Tendega, Katibu wa Bawacha; Conchesta Rwamlaza, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Kagera na Anatropia Theonest; Mbunge Viti Maalum jana walikamatwa na kuhojiwa ambapo Mdee pekee hakupewa dhamana.

Awali, Polisi waligoma kumpa dhamana Mdee wakidai wanasubiri maelekezo kutoka kwa Kamanda wa Mkoa wa Kagera, aliyekuwa kwenye ziara ya Rais John Magufuli.

Taarifa iliyotolewa Chadema imeeleza kuwa, Mdee amedhaminiwa na watu wawili ambapo pia ametakiwa kuripoti kituoni hapo baada ya mwezi mmoja au wakati wowote polisi watakapomuhitaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!