Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee aivuruga serikali, waziri amvaa
Habari za SiasaTangulizi

Mdee aivuruga serikali, waziri amvaa

Halima Mdee
Spread the love

 

HALIMA Mdee, mbunge asiye na chama bungeni, amekosoa Mpango wa Maendeleo wa Serikali, kwamba ‘hakuna kitu.’ Anaripoti Mwandshi Wetu, Dodoma…(endelea).

Akichangia mpango huo tarehe 9 Februari 2021, Mdee ambaye alifukuzwa Chadema kwa tuhuma za usaliti amesema, mpango huo hautekelezeki.

Ameeleza kushangazwa na wabunge kuufurahia mpango huo huku akisisitiza, hauna jipya katika kukuza uchumi wa nchi.

“Ukuaji wa uchumi hamna kitu, uwiano wa pato la mtu hakuna kitu, kiwango cha umasikini ni kikubwa. Hapa shida ni wataalamu wetu halafu ninyi mnacheka na kushangilia,” amesema Mdee.

Amefafanua kwamba kuna shida kwa upande wa watalaam wa serikali, huku akipendekeza serikali kujikita zaidi kuwekeza kwenye kilimo kwa maslahi ya Watanzania wengi.

Mdee alieleza kushangazwa na wabunge kuusifu mpango huo huku ukiwa huna jipya na kwamba kuna mabadiliko machache tu.

Mchango huo wa Mdee ulimsukuma Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu ambaye mara mbili aliomba kumpa taarifa Mdee kupinga kile alichokuwa akieleza.

Akijibu hoja ya Mdee kwamba ‘hakuna kitu,’ Mhagama amesema, vitu alivyokuwa akizungumza Mdee, serikali imevifanya.

Waziri huyo alisisitiza, kwamba mchangiaji (Mdee) hakuwa na sababu ya kuzungumza yale aliyokuwa akizungumza kwa kuwa yalikuwa yamefanyiwa kazi na serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!