Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mchungaji atoa neno ‘watu wasiojulikana’
Habari Mchanganyiko

Mchungaji atoa neno ‘watu wasiojulikana’

Michael Nhonya akifundisha somo la Uongozi kwneye Kongamano la Vijana Taifa June, 2017
Spread the love

KANISA la Wabaptist Tanzania limewataka viongozi wa serikali pamoja na vyama vya siasa kuhakikisha wanakuwa mabalozi wa kulinda amani ya nchi, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo limetolewa huku kukiwa na wimbi la kuwapo matukio mbalimbali ya uhalifu yakiwamo ya watu kuvamiwa na kupigwa risasi na ”watu wasiojulikana”

Makamu mwangalizi mkuu wa Kanisa la Wabaptist Tanzania (BCT) Mchungaji, Michael Nhonya, alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akihubiri katika ibada iliyofanyika kanisani hapo eneo la Makole mkoani Dodoma.

Amesema kuwa hali ya wasiwasi inayojitokeza kutokana na vitendo ambavyo vinavyoashiria kupoteza amani ni muhimu vyombo hivyo  vikasaidia kudumisha amani ya nchi.

Amesema ili kukabiliana na vitendo hivyo visiendelee kujitokeza kuna haja ya serikali kuingilia kati na kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini wahalifu hao.

Amesema kuwa  kanisa hilo kamwe halitaweza kuvivumilia vitendo hivyo bila kuvikemea.
Ameongeza kuwa bado wanaamini nchi ya Tanzania ni ya amani na utulivu.

“Sisi kama viongozi wa dini tutaendelea kukemea kila mtu bila kujali cheo chake, tutasema na kuelekeza inapobidi kufanya hivyo”, amesema.

Amewataka  Watanzania kuwa na subira wakati vyombo vya dola nchini vikiendelea kuchunguza matukio yanayotokea kwa sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!