Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mchungaji Anglikana atuhumiwa kusafirisha meno ya Tembo
Habari Mchanganyiko

Mchungaji Anglikana atuhumiwa kusafirisha meno ya Tembo

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

SHEKANDI Ashery Mkombola (44), Mchungaji wa Kanisa la Aglikana, lililopo katika Kijiji cha Chinyika, Mpwapwa jijini Dodoma, na watu wengine 21 wanatuhumiwa kukutwa na vipande18 vya meno ya Tembo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto, watuhumiwa hao walikamatwa katika matukio mawili tofauti, ambapo mchungaji Mkombola amedaiwa kukutwa akisafirisha meno mawili ya Tembo yenye uzito wa kilogram 15.

“Mchungaji huyu alikamatwa katika Kijiji cha Pwaga, kilichopo tarafa ya Kibakwe ingawa anaishi Kijiji cha Mungui na alikua akisafirisha meno hayo kwa kutumia pikipiki aina ya Fekon, yenye namba za usajili MC 772 AYK,” amefafanua Kamanda Muroto.

Amesema, katika tukio la pili watuhumiwa wawili ambao majina yao yanahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi, wamekamatwa katika stendi ya mabasi ya nane nane jijini Dodoma wakiwa na vipande 16 vya meno ya Tembo, wakiwa wamevificha katika dumu la lita 20 lililokatwa juu.

Katika tukio jingine, Kamanda Muroto amesema polisi inawashikilia watu wawili – Sam Ally Isihaka (44), dereva wa gari aina ya Benz lenye namba za usajili AIB 5596 na Mwinyi Ramadhani Magumila (47), dereva wa gari aina ya Benz lenye namba za usajili AIB 6924 kwa kosa la kukwepa ushuru.

Amesema, watuhumiwa hao wakiwa safarini kuelekea Rwanda, walikwepa ushuru wa serikali katika mizani ya Uyole Mbeya, Makambako, Njombe na Wenda Tanangozi Iringa kwa kushawishi na kutoa rushwa kwa maofisa wa mizani.

“Maafisa hawa wa mizani nao walipokea rushwa na kutoa risiti bandia, ili kuruhusu magari hayo mali ya kampuni ya Reginal Logistics ya Dar es Salaam kupita bila kupima. Walikuwa wamezidisha uzito wa mizigo zaidi ya 650 grm yaani gross vehicle mass,” amebainisha Kamanda Muroto.

Kufuatia tukio hilo, Muroto amesema watuhumiwa sita wakiwemo maofisa wa mizani waliokuwa zamu katika vituo hivyo, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na wanatarajia kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!