Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mchezaji wa zamani wa Taifa Zambia, Kaizer Chiefs afariki kwa kushambuliwa na mbwa wake
Kimataifa

Mchezaji wa zamani wa Taifa Zambia, Kaizer Chiefs afariki kwa kushambuliwa na mbwa wake

Philemon Mulala
Spread the love

 

NYOTA wa zamani wa Chipolopolo, Philemon Mulala amefariki dunia baada ya kuumwa na mbwa wake watatu nyumbani kwake Lichtenburg Afrika Kusini. Yameripoti Mashirika ya Habari ya Kimatiafa … (endelea).

Taarifa zinaeleza kuwa Mulala aliumwa na mbwa hao alipotoka nje kuchunguza kwanini walikuwa wanabweka sana baada ya umeme kukatika.

Msemaji wa polisi, Sam Tselanyane, ameiambia BBC kuwa mke wake aliwaambia kwamba alisikia mbwa wakibweka lakini hakujishughulisha na kwenda kuangalia ni nini kilikuwa kibaya kwani mbwa hao mara kwa mara walikuwa wakiwabwekea watembea kwa miguu na magari yaliyokuwa yakipita.

“Baada ya umeme kurudi, aliingia ndani ya nyumba hiyo akimtafuta mumewe lakini hakumpata, baada ya kuendelea na upekuzi, mwanamke huyo alimuona mumewe akiwa amelala nje kwenye bustani. Kisha akatoka nje kupeleleza kulikoni, na akagundua mume wake alikuwa hatikisiki baada ya kuumwa na mbwa wao watatu.”

Mamlaka zimewaondoa mbwa hao wawili ambao ni ‘Cross breed” ya Pitbul na mbwa wa tatu hajulikani asili yake ila anasemekana kuwa mkali.

Mulala alihamia Afrika Kusini kuichezea klabu ya Kaizer Chiefs mwaka wa 1988. Pia alichezea Cape Town Spurs na Lenasia Dynamos.

Shirikisho la soka la Zambia (FAZ)limetoa taarifa ya kuomboleza kifo cha Mulala likisema alikuwa sehemu ya kikosi cha Zambia cha mwaka 1984 kilichoshinda Kombe la East and Central Africa Challenge chini ya ukufunzi wake kanali Brightwell Banda.

Katibu Mkuu wa FAZ Adrian Kashala amesema chama cha soka kimepoteza mchezaji hodari.

Tunabaki na kumbukumbu nzuri ambazo marehemu Philemon alituheshimu nazo uwanjani. Kuna mengi ambayo wachezaji wa leo wanaweza kujifunza kutoka kwa kizazi cha marehemu,” Kashala alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!