Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Mchakato wa kocha mpya Simba wafikia patamu, Mmorocco apewa nafasi
HabariMichezo

Mchakato wa kocha mpya Simba wafikia patamu, Mmorocco apewa nafasi

Erradi Mohammed Adil
Spread the love

 

NI kama mchakato wa kumtafuta kocha mpya wa klabu ya Simba umeendelea kupamba moto, kufuatia mpaka sasa uongozi wa klabu hiyo kupokea wasifu wa makocha zaidi ya 100, huku kocha wa sasa wa APR ya Rwanda Erradi Mohammed Adil raia wa Morocco, akipewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Simba imejikuta kwenye mchakato huo, mara baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wao Pablo Franco Martini raiaa Hispania, ambaye alitimuliwa na uongozi wa klabu hiyo kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Simba katika msimu huu.

Kocha huyo raia wa Morocco anapewa nafasi kubwa, kutokana na viongozi wa klabu ya Simba kumtaka kocha ambaye analijua vizuri soka la barani Afrika, na hivyo mmoja ya vigezo vyao ni kuchagua kocha ambaye anatoka ndani ya bara la Afrika.

Vigezo hivyo vinathibitisha na manane aliyonukuliwa mtendaji wa klabu ya Simba katika siku za hivi karibuni kupitia Simba App, na kusema kuwa, kwa sasa wanahitaji kocha mzawa wa bara la Afrika.

“Tunahitaji Kocha anayejua vizuri soka la Afrika pia tungefurahi kupata Kocha ambaye ni mzawa wa bara hili lakini mpaka sasa bado hawajatuma wasifu na aliteyuma mmoja na vigezo vyake havitoshi” alisema Barbara

Akizungumzia idadi ya wasifu waliopokea mpaka sasa, mtendaji huyo alisema kuwa wapokea wasimu wa makocha zaidi ya 100 huku wengi wao wakitokea barani Ulaya, lakini mchakato huo huwenda ukakamilika wiki mbili zijazo.

“Tumepokea wasifu wa makocha zaidi ya 100 kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao wengi wao ni kutoka barani Ulaya na Amerika Kusini. Mchakato wa mchujo unaendelea na tunategemea utakamilika ndani ya wiki mbili zijazo” Alisema Barbara

Barbara Gonzalez, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba

Kuelekea msimu ujao, klabu hiyo imedhamilia kufanya mabaliko makubwa kwenye benchi lao la ufundi, kufuatia kumaliza msimu huuu bila taji lolote.

Simba iliamua kumtimua Pablo siku chache mara baada ya kupoteza mchezo wa nusu fainali ya kombe la Shirikisho la Azam, dhidi ya Yanga ambao ulipigwa kwenye dimba la CCM kirumba, Mwanza.

Makubaliano ya Simba kumvunjia kocha huyo mktaba, yalifikiwa Mei 31 mwaka huu, na klabu hiyo ilimtakiwa kila la kheri katika maisha yake mapya nje ya klabu hiyo.

Pablo alijiunga na Simba tarehe 10 Novemba 2022, Akichukua nafasi ya Didier Gomes, ambaye aliamua kuachana na timu hiyo kufutai matokeo mabaya aliyoyapata kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kwenye msimu huu.

Toka alipofika nchini Pablo amefanikiwa kuwapa Simba taji moja tu, la michuano ya kombe la Mapinduzi mara baada ya kuwafunga Azam FC kwenye fainali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!