Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Mburkina Faso atua kumrithi Kapombe Simba
Michezo

Mburkina Faso atua kumrithi Kapombe Simba

Zana Coulibaly
Spread the love

MCHEZAJI Zana Coulibaly raia wa Burkina Faso anatarajia kutua leo nchini kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usajili na Simba akitokea timu ya ASEC Mimosas kwa ajiri ya kuongeza nguvu ndani ya kikosi hicho. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Coulibaly ambaye anakuja kuziba nafasi ya Shomari Kapombe ambaye amepata maumivu ya mguu alipokuwa kwenye kambi ya timu ya taifa nchini Afrika Kusini, hivyo anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Simba kupitia kwenye ukurasa wa kwenye mtandao wao wa kijamii wa Instagram wamethibitisha ujio wa mchezaji huyu ndani ya kikosi cha kama sehemu ya kukifanyia maboresho kuelekea michezo ya ligi kuu bara na ile ya klabu bingwa Afrika.

“Tunapenda kuwatangazia kwamba beki Zana Coulibaly kutoka ASEC Mimosas ya Ivory Coast leo atawasili nchini kwa ajili kukamilisha taratibu za mwisho kujiunga na timu yetu ili kuziba pengo la beki Shomari Kapombe ambaye siku za karibuni alipata majeraha.”

Simba huu ndiyo utakuwa usajili wao wa kwanza toka kufunguliwa kwa dirisha dogo la usajiri 15, Novemba, 2018, huku leo wakitarajia kucheza mcherzo wao wa hatua ya awali ya michuano ya kombe la Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Mbambane Swallows kutoka Swaziland kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!