MBUNGE wa Ukonga Mwita Waitara (Chadema) amembana Naibu Spika, Dk.Tulia Akson na kumtaka atangaze kuwa anautambua uongozi wa gani wa wabunge wa CUF ndani ya Bunge, anaandika Dany Tibason.
Waitara alimbana Naibu Spika wakati akiomba mwongozi wa Spika ili kutaka lijua msimamo wa Spika wa kutambua uongozi halali wa viongozi wa CUF ndani ya Bunge.
“Spika,Masuala ya CUF ndani ya bunge yameleta kizungunkuti kila mmoja anajua kuwa leo hii Spika ametangaza kutambua uongozi ulioletwa na wabunge wanaotokana na upande wa pili licha ya kuwepo kwa mgogoro.
“Leo tunataka Spika atoe mwongozo wa Bunge linawatambua viongozi gani ili kuhakikisha mzozo huo unaisha badala ya kuwepo mzozo usioisha ili lijulikane moja “ alihoji
Hata hivyo, Naibu spika amesema hawezi kutoa majibu ya mwongozo huo kwani anatakiwa kusikiliza vyema maelezo ya Spika juu kuwatambua viongozi wa Bunge wa CUF wanaotokana na kambi ya pili.
Awali Chama cha Wananchi (CUF), upande wa mwenyekiti Prof.Ibrahim Lipumba kilitangaza kuunda kambi yao bungeni tofauti na iliyokuwapo inayoundwa na UKAWA.
Bunge lilielezwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF bara, Magdalena Sakaya ambaye ni mbunge wa Kaliyua aliwasilisha majina ya viongozi wapya wa chama hicho kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Katika majina yaliyowasilihswa kwa Spika wa Bunge ni pamoja na jina la mbunge wa Mtwara Mjini ambaye amechaguliwa kushika nafasi ya mwenyekiti wa wabunge wa CUF bungeni.
Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, aliwaambia wabunge leo bungeni kuwa ofisi ya Spika ilipokea orodha mpya ya viongozi wa CUF 8 Agosti, mwaka huu na kueleza kuwa chama hicho kinautambua uongozi huo kwa sasa.
Kwa sasa mwenyekiti wa CUF ni mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea ambaye anaunga mkono uongozi wa Maalim Seif na kupinga uongozi wa Prof.Lipumba.
“Mnamo Septemba 8, mwaka huu, ofisi ya Spika imepokea ripoti kutoka kwa Sakaya na kuonyesha mabadiliko yaliyofanywa na mkutano wa chama hicho Septemba 6, mwaka huu.
“Kulingana na mabadiliko mapya, Nachuma anakuwa mwenyekiti wakati mbunge wa viti maalum Rukia Kassim Ahmed ni Katibu wa chama bungeni” alieleza Dk Tulia.
Hata hivyo, Mbunge wa Malindi Ally Saleh (CUF) alikataa mabadiliko hayo kwa kutumia nafasi ya kuomba mwongozo wa Spika.
Ally Salehe aliomba mwongozo wa Spika akisema kuwa wabunge wa chama hicho wakiwa zaidi 40 walichagua viongozi na kwamba walipoondoka wabunge nane kulibaki nafasi zilizowazi.
Amesema walishafanya uchaguzi wa kujaza nafasi hizo ikiwemo nafasi ya uenyekiti iliyoachwa wazi na Riziki Ngwali na walimchagua Mbunge wa Temeke, Abdalah Mtolea.
Akahoji ni nani anayeamua kuhusu uongozi wa wabunge bungeni ni wabunge wachache ama walio wengi.
Pia alitaka kufahamu kwa sababu wao wameshafanya uchaguzi inawezekana kuwa na uongozi juu ya uongozi.
Akijibu Dk Tulia amesema Spika amepokea taarifa ya viongozi hao, lakini hajapokea taarifa ya uchaguzi wa upande wakina Ally Salehe.
Amesema watakapoleta taarifa yao ndipo Spika ataamua.
Leave a comment