Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aiwakia serikali
Habari za Siasa

Mbunge Chadema aiwakia serikali

Ziwa Victoria
Spread the love

HATUA ya serikali kuahidi miradi mikubwa na kisha kuitekeleza, imemkera Gimbi Masaba, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema). Anaripoti Dandoson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Masaba ameitaka serikali kueleza ni kwanini imekuwa ikipanga kutekeleza miradi ambayo hawatekelezeki?

Akiuliza swali la nyongeza leo tarehe 3 Mei 2019 bungeni amesema kuwa, licha ya kuwa serikali imekuwa ikitoa miradi mingi mikubwa lakini haitekelezeki.

“Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria yana mabomba makubwa mawili ambapo moja lilikuwa la maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya kunywa, na bomba la pili lilikuwa la maji ya kawaida kwa ajili ya mifugo na mengineyo.

“Sasa nataka kujua mkataba huo umezingatia ufanisi wa mradi huo. Tumekuwa na miradi mingi ambayo tunayo katika bajeti ambayo hivi sasa inaelekea kuishia, sasa nataka kujua miradi ya Nyang’okolwa, Nyakabindi, Sanungu na mradi wa mhina haijatekelezwa, je mpaka lini?” amehoji.

Amsema kuwa, miradi hii bado haijatekelezeka, na kwenye kitabu cha Waziri wa Wizara ya Maji nimeona kuna miradi 10 ambayo imepelekwa Simiyu.

“Sasa nataka kufahamu, ni kwa nini serikali inatoa miradi ambayo haitekelezeki?” amehoji Masaba.

Awali, katika swali la mbunge huyo ni lini serikali itatekeleza ahadi ya kujenga mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Viktoria kuanzia Nyashimo, Ngasamo, Dutwa, Bariadi, Bariadi, Itilima, Meatu na Maswa.

Akijibu maswali hayo Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema kuwa, serikali serikali itahakikisha inakamilisha miradi mingi ambayo imeahidiwa.

Aidha amesema, serikali imetoa Sh. 44 Bil za kuwalipa watu ambao walitakawa kulipwa fidia zao.

aidha Awesso amesema kuwa, miradi yote ambayo imeahidiwa na serikali itatekelezwa na tatizo kubwa ilikuwa kukwama katika ulipwaji.

Na kwamba, baada ya kupata fedha za kulipa fidia, watu wanaotaka zaidi ya Sh. 44 Bil na imepatikana Sh. 5 Bil kwa ajili ya kukamilisha miradi.

Amesema kuwa, ni kweli serikali itatekeleza mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka katika Nyashimo (Busega), Bariadi, Lagangabilili, Maswa na Mwanhuzi.

Aidha Awesso alisema kuwa kwa awamu zote kutawanufaisha wananchi wapatao 834,204.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!