Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko
Habari za Siasa

Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko

Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma
Spread the love

MBUNGE Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema) ameitaka serikali kutoa taarifa ya masoko kwa wafanyabiashara ya mahindi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwakajoka alitoa kauli hiyo Bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza, amesema kuwa serikali imekuwa na tabia ya kuwazuia wafanyabiashara wa nafaka nje kwa kisingizio cha njaa. 

Aidha Mwakajoka ametaka kujua kama serikali ina mpango wa kuwatangazia masoko kwa kuwa bunge halionyeshwi moja kwa moja kutokana na hilo wafanyabiashara hawawezi kujua masoko yalipo.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa kuna chakula cha kutosha nchini hivyo ruksa kuuza chakula kwenye masoko ya nje.

Aidha Mhandisi Manyanya amesema kuwa wafanyabiashara wanaotafuta masoko wapitie wizara husika kwa kutumia simu au njia ya mitandao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!