Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko
Habari za Siasa

Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko

Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma
Spread the love

MBUNGE Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema) ameitaka serikali kutoa taarifa ya masoko kwa wafanyabiashara ya mahindi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwakajoka alitoa kauli hiyo Bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza, amesema kuwa serikali imekuwa na tabia ya kuwazuia wafanyabiashara wa nafaka nje kwa kisingizio cha njaa. 

Aidha Mwakajoka ametaka kujua kama serikali ina mpango wa kuwatangazia masoko kwa kuwa bunge halionyeshwi moja kwa moja kutokana na hilo wafanyabiashara hawawezi kujua masoko yalipo.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa kuna chakula cha kutosha nchini hivyo ruksa kuuza chakula kwenye masoko ya nje.

Aidha Mhandisi Manyanya amesema kuwa wafanyabiashara wanaotafuta masoko wapitie wizara husika kwa kutumia simu au njia ya mitandao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!