MBUNGE wa Jimbo la Namtumbo, Vita Kawawa (CCM) amepata ajali katika eneo la Nalasi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wakati akiwa kwenye ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Ndugu Christina Mndeme ambaye ana ziara leo huko Namtumbo, mkoani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).
Taarifa zilizofikia Mwanahalisi Online ni kwamba katia ajali hiyo iliyotokea leo mchana, Mbunge huyo aliyekuwa na watu wengine watatu kwenye gari na wote wametoka salama.
Aidha, akizungumza na MwanaHalisi Online, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Simon Maigwa amesema bado hajapata taarifa rasmi kuhusu ajali hiyo kwa kuwa naye yumo kwenye msafara wa ziara hiyo.
Leave a comment