Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM amwaga ahadi akiwania uspika
Habari za Siasa

Mbunge CCM amwaga ahadi akiwania uspika

Spread the love

 

MBUNGE wa Mlimba (CCM), Mkoa wa Morogoro, Godwin Kunambi amechukua fomu za kuwania kurithi mikoba ya Job Ndugai ya uspika wa Bunge la Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kunambi amechukua fomu hiyo Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma leo Jumatatu, tarehe 10 Januari 2022 akisema ana uzoefu wa kutosha kuongoza muhimili huo wa Bunge.

“Nimesukumwa na hali ya kutimiza haja yangu ya msingi, nina sifa za kuwa Spika wa Bunge la Tanzania,” amesema

Kunambi amesema, “nimehudumu kama mwanasheria wa CCM kwa miaka mitano. Nimehudumu kama mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kilana nimejipima sifa na uwezo ninao.”

“Ninawaahidi wabunge kwamba nitakwenda kusimamia uhuru na usawa kwa wabunge wote.”

Kunambi anaungana na Mbunge wa zamani wa Shinyanga Mjini, Stephen Masele kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho cha uspika ambapo fumo zimeanza kutolewa leo hadi 15 Januari 2022.

Mchakato huo umetangazwa baada ya Job Ndugai kutangaza kujizulu nafasi hiyo wiki iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!