Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM akumbushia ahadi ya Magufuli bungeni
Habari za Siasa

Mbunge CCM akumbushia ahadi ya Magufuli bungeni

Bunge la Tanzania
Spread the love

AHADI aliyoitoa Rais wa Tanzania, John Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2020, Itigi mkoani Singida, kwamba atajenga barabara za kilometa 10, imeibuliwa bungeni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Akiuliza kuhusu ahadi hiyo leo Jumatatu tarehe 8 Februari 2021, Yahaya Masare, Mbunge wa Manyoni Magharibi (CCM), ameuliza wakati utekelezaji huo utaanza.

“Wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2020, Mhe. Rais akiwa katika Mji wa Itigi, aliahidi ujenzi wa barabara kwa kilometa 10 katika Mji huu. Je,ni lini utekelezaji wa ahadi hiyo utaanza?” ameuliza.

Naibu Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Dk. Festo Dugange amesema, inaendelea kuboresha miundombinu katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Itigi.

Rais John Magufuli

Na kwamba, katika Mwaka wa Fedha 2019/20, serikali ilijenga barabara yenye urefu wa kilometa 1.1 kwa kiwango cha lami kuzunguka Stendi Kuu ya Mabasi, Itigi kwa gharama ya Sh. 499.87 milioni.

“Serikali imekamilisha usanifu wa barabara zenye urefu wa kilomita 10 kwa kiwango cha lami eneo la Itigi, ambazo zitagharimu kiasi cha Sh.9.5 bilioni.”

“Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2020/21, kiasi cha Sh.686.8 bilioni kimetengwa kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 101.36 ambapo mpaka sasa kiasi cha Shilingi 253.97 bilioni kimetolewa na utekelezaji unaendelea,” ameema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!