Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM aivimbia serikali
Habari za Siasa

Mbunge CCM aivimbia serikali

Maryprisca Mahundi, Naibu Waziri wa Maji
Spread the love

 

NICODEMUS Maganga, Mbunge wa Mbogwe kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM), amegomea majibu ya serikali, kwamba jimboni kwake serikali imechimba visima virefu vya maji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mganga alipinga majibu hayo baada ya Maryprisca Mahundi, Naibu Waziri wa Maji leo tarehe 14 Aprili 2021, kusema serikali imechimba visima 26 jimboni humo na kuwa, vinatumika mpaka sasa.

“Sijaridhishwa na majibu ya serikali, hivyo visima vimechimbwa wapi?” amehoji Manga na kuongeza “mimi ni mbunge wa Mbogwe na ninaishi huko, lakini sijawahi kuona hayo maji naomba kujua visima viko wapi?”

Mbunge huyo amelieleza Bunge, kwamba wananchi wake wanaendelea kuteseka kwa adha ya maji, akisitiza majibu ya waziri huyo ni ya kwenye makaratasi.

Hata hivyo, Waziri Mahundi ameahidi kuongozana na mbunge huyo jimboni kwake, ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezekano wa kutumia maji ya Ziwa Victoria kukabili shida hiyo ya maji.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!