Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ataka walioporwa fedha na TRA warejeshewe
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge ataka walioporwa fedha na TRA warejeshewe

Mbunge wa Vunjo mkoani Kilimanjaro (CCM), Dk. Charles Kimei
Spread the love

 

MBUNGE wa Vunjo mkoani Kilimanjaro (CCM), Dk. Charles Kimei, ameiomba Serikali irudishe fedha za kodi zilizokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwenye taasisi za dini, kinyume cha sheria. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Akizungumza bungeni jijini Dodoma, leo Jumanne tarehe 25 Mei 2021, Dk. Kimei amedai kuwa, utendaji wa taasisi hizo umezorota, baada ya kushinikizwa na baadhi ya maafisa wa TRA, walipe kodi.

Wakati huo huo, Dk. Kimei, aliiomba Serikali iwachukulie hatua maafisa hao, wanaodaiwa kuzishinikiza taasisi za dini, kulipa kodi kinyume cha sheria.

“Serikali itakuwa tayari kurejesha kodi zilizokusanywa katika taasisi hizo kwa shinikizo na hatimaye kuzidhoofidha sana? Pili, Serikali iko tayari kuchukua hatua za kinidhamu kwa maafisa wa TRA wanaokiuka sheria?” amesema Dk. Kimei.

Mbali na maombi hayo, Dk. Kimei aliiomba Serikali isamehe madeni ya kodi za muda mrefu, ya taasisi za dini, zilizokuwa zinajiendesha kwa utaratibu wa kutopata faida.

“Je, Serikali haioni umuhimu wa kuzisamehe kodi za miaka ya nyuma taasisi za dini, zilizokuwa zikiendeshwa kwa utaratibu usiolenga kupata faida. Na kuziwekea utaratibu wa kuanza kulipa tangu walipojulishwa utaratibu wa kuanza kulipa kodi?” amesema Dk. Kimei.

Akijibu maombi hayo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali itafanyia kazi maombi hayo, na ikibainika taasisi hizo zilitozwa kodi kinyume cha sheria, itazirejesha fedha hizo.

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

“Serikali ina utaratibu wa kurejesha fedha ambazo zilichukuliwa na kwa mujibu wa sheria, inatakiwa kurejeshwa kwa utaratibu wa kawaida wa kufanya refunding,” amesema Dk. Nchemba.

Kuhusu maafisa TRA wanaodaiwa kukiuka sheria, Dk. Nchemba amesema Serikali itafanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na kwamba ikibainika wana makosa, itawachukuliwa hatua za kinidhamu.

“Na meneo ambayo kuna amkosa ya ukiukwaji sheria, taratibu za kisheria hufuatwa na hatua stahiki za kinidhamu huchukuliwa kwa wanaokiuka sheria. Kama kuna meneo maafisa wetu wamekiuka sheria, taratibu za kisheria zitachukuliwa,” amesema Dk. Nchemba.

Akizungumzia ombi la taasisi hizo kusamehewa madeni, Dk. Nchemba amesema Serikali inaendelea kufanya tathimini juu ya maombi hayo, kwa ajili ya kuchukua hatua.

“Serikali imekuwa ikipokea maombi ya kusamehe kodi za miaka ya nyuma toka taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na taasisi za Dini. Serikali inaendelea kutathmini maombi hayo, ili kuona hatua zinazoweza kuchukuliwa bila kuathiri matakwa ya sheria zilizopo,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!