Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mbunge ashangazwa wananchi kuzuiwa kujenga shule
Elimu

Mbunge ashangazwa wananchi kuzuiwa kujenga shule

Wanafunzi wakiwa darasani
Spread the love

MBUNGE wa Chilonwa, Joel Makanyaga (CCM) ameshangazwa na Serikali kutoruhusu wananchi kujenga shule wenyewe hata madarasa mawili kila mwaka ili kupunguza masangamano wa wanafundi madarasani. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mbunge huyo amesema, shule nyingi za msingi  nchini Tanzania zina wanafunzi wengi wanaozidi kiwango kinachotakiwa cha wanafunzi takribani 700.

Kutokana na hali hiyo, mbunge huyo alisema ni kwa nini, Serikali isiruhusu wananchi wajenge shule nyingine kwa mpango wa kujenga hata madarasa mawili kila mwaka na shule hizo zikatambuliwa kisheria.

Akijibu swali hilo, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Tamisemi amesema,  wananchi wanaruhusiwa kujenga shule katika maeneo yenye mahitaji kwa kushirisha viongozi wa Halmashauri ili kusogeza huduma karibu na wananchi.

Amesema kupitia utaratibu huo, Serikali imefanikiwa kuwa na shule ya msingi kila Kijiji na Shule za Sekondari kila Kata.

Aidha, amesema,  Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi imekuwa na utaratibu wa kujenga vituo shikizi katika maeneo ambayo shule mama iko mbali ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Amesema, serikali kutokana na kuwepo kwa vituo hivyo, baadhi ya vituo hivyo baadaye husajiliwa kuwa shule baada ya kukidhi vigezo vinavyotakiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!