Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mbunge alilia walimu wa kike shule Birise, Donsee
Habari

Mbunge alilia walimu wa kike shule Birise, Donsee

Spread the love

 

KUNTI Majala, Mbunge Viti Maalumu mkoani Dodoma, ameiomba serikali kupeleka walimu wa kike katika Shule za Msingi Birise na Donsee, zilizoko mkoani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Majala ametoa ombi hilo leo Alhamisi tarehe 4 Februari 2021 bungeni jijini Dodoma, ambapo ameihoji Serikali lini itapelek walimu wa kike katika shule hizo ambazo hazina walimu hao.

Akijibuwa ombi hilo, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, ameeleza kwamba serikali inatambua changamoto hiyo na kwamba inajiandaa kuweka mpango wa ajira na mgawanyo wa walimu wapya katika halmashauri zote nchini.

Aidha, TAMISEMI imeagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha inaweka idadi sawa ya walimu kwa kuzingatia jinsia.

“Wakati serikali ikijiandaa na mpango wa ajira na mgawanyo wa walimu wapya, Ofisi ya Rais-TAMISEMI inazielekeza Halmashauri zote nchini kufanya msawazo wa walimu wa Shule za Msingi na Sekondari,” ameagiza.

Hata hivyo, Waziri wa TAMISEMI amesema wizara yake imepeleka mwalimu mmoja wa kike katika Shule ya Msingi Donsee, wakati ikiendelea kukamilisha taratibu za kumpeleka mwalimu wa kike katika Shule ya Msingi Birise.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

error: Content is protected !!