Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge akerwa mawaziri “kuchati” bungeni, aomba mwongozo
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge akerwa mawaziri “kuchati” bungeni, aomba mwongozo

Spread the love

MBUNGE wa Songwe, Philipo Mulugo, ameomba mwongozo bungeni jijini Dodoma, juu ya tabia ya baadhi ya mawaziri wanaodaiwa kutumia simu (kuchati na kuongea na simu), wakati wabunge wanaendelea kuchangia masuala ya msingi juu ya mustakabali wa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Mulugo ameomba mwongozo huo leo tarehe 3 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, wakati Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara anatoa mchango wake kuhusu taarifa za kamati za kudumu za Bunge, juu ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 2022.

Mbunge huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amedai wakati Waitara anatoa mchango wake, baadhi ya mawaziri walikuwa wanachati kama anayoyazungumza hayawahusu.

“Mheshimiwa mwenyekiti, kama mbunge wa CCM moyo unaniuma mbunge mwenzetu anapochangia taarifa kama hii, inauma kuona wanaohusika mawaziri wanachati na simu, wanaongea na simu hawajali kile ambacho anakiongea Waitara. Kama vile jambo linapita, haomba mwongozo wako,” amesema Mulugo.

Baada ya Mulugo kutoa ombi hilo, Mwenyekiti wa Bunge, Daniel Sillo, alisema mwongozo kuhusu suala hilo utatolewa baada ya kikao hicho kuisha.

Wakati waitara anachangia, alitaka sheria itungwe ili kuwanyonga watu watakaobainika pasina shaka kuwa ni wezi wa mali za umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!