Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge aiomba Serikali isamehe madeni ya wafanyabiashara
Habari Mchanganyiko

Mbunge aiomba Serikali isamehe madeni ya wafanyabiashara

Mashine ya EFD
Spread the love

 

MBUNGE wa Mbogwe mkoani Geita (CCM), Henry Maganga, ameiomba Serikali iwafutie madeni wafanyabiashara, wenye madeni yanayotokana na ukosefu wa elimu juu ya matumizi sahihi ya Mashine za Risiti za Kielektroniki (EFD). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Maganga ametoa ombi hilo leo Ijumaa tarehe 21 Mei 2021, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

“Bado wafanyabiashara wana kilio hapa nchini, hawana furaha na Serikali yao. Hawakuwa na elimu juu ya mashine ya EFD, naomba Serikali itoe kauli ili nchi ijue wamesha samehewa madeni,” amesema Maganga.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhandisi Hamad Masauni, amesema Serikali itafanya tathimini juu ya maombi hayo, ili kujua faida na athari zake, endapo itasamehe madeni hayo.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamadi Masauni

“Kauli ya Serikali kuhusu kusamehe madeni haiwezi kutolewa kwa utaratibu huu, msamaha wa madeni uko kwa mujibu wa sheria . Kwa hiyo hatuwezi kusimama hapa tukatoa tamko kusema tunamsamehe nani madeni,” amesema Mhandisi Masauni na kuongeza:

“Ili msamaha utoke lazima tukae chini kufanya tahimini na utafiti wa kina, kuona athari na faida za kufanya hivyo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!