Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji wanafunzi Veta kukosa mikopo, waziri amjibu
Habari za Siasa

Mbunge ahoji wanafunzi Veta kukosa mikopo, waziri amjibu

Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum (Chadema), Zubeda Sakuru, ametaka kujua kwa nini wanafunzi wanaojiunga na vyuo vya ufundi stadi (Veta) kukosa mikopo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea)

Zubeda ameuliza swali bungeni leo Alhamisi tarehe 28 Mei, 2020 kwa njia ya mtandao na kujibiwa na mfumo huo huo na waziri wa elimu, sayansi na teknolojia.

“Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaojiunga na vyuo vya ufundi stadi (Veta), lakini wanafunzi waliojiunga na vyuo hivyo hawapati mikopo kutoka serikalini. Je, Serikali itaanza lini kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vya ufundi stadi,” ameuliza Zubeda.

Akijibu swali hilo, waziri wa elimu, sayansi na teknolojia amesema, kwa sasa mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (SURA 178) ambayo inawabainisha walengwa ni Watanzania wahitaji walioomba mkopo na wenye sifa za kujiunga na taasisi za elimu ya juu na sio vyuo vya ufundi stadi.

Serikali imeendelea kutambua kuwepo kwa umuhimu mkubwa wa mafunzo ya ufundi stadi kama kipaumbele chetu cha kujenga uchumi wa viwanda.”

“Hivyo, Serikali imeendelea kubeba gharama nyingi za vyuo vya ufundi stadi vya Serikali ambavyo havilengwi na sheria hiyo ili ada zao ziwe nafuu na Watanzania wa kawaida waweze kumudu,” amesema

Amesema, Serikali inaendelea kupanua upatikanaji wa fursa hizo za masomo hayo ya ufundi stadi kwa kujenga vyuo vipya hasa maeneo ya vijijini ambayo yalikuwa hayana vyuo hivi.

“Kwa sasa, utaratibu utaendelea kuwa huo huo wa Serikali kuvipa vyuo hivyo vya ufundi stadi ruzuku ili kumpunguzia mwananchi wa kawaida gharama za kusoma.”

“Hata hivyo, maoni ya Zubeda Sukuru na wadau wengine yanaendelea kupokelewa ili kuboresha utaratibu wa sasa kwa kadri uchumi wetu unavyoendelea kuimarika,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!