Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji ubovu barabara za Singida, Serikali yamjibu
Habari za Siasa

Mbunge ahoji ubovu barabara za Singida, Serikali yamjibu

Spread the love

 

AYSHAROSE Mattenbe, Mbunge viti maalumu (CCM), ameitaka serikali kuona umuhimu wa kuzijenga barabara zinazounganisha jimbo la Singida Kaskazini mkoani humo. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Ameyasema hayo leo Jumanne, tarehe 18 Mei 2021, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

Mbunge huyo amesema, serikali inapaswa kutambua umuhimu wa barabara hiyo kwa sababau ndiyo inayoonganisha vijiji vyote vya Singida Kaskazini.

“Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za Singida Kaskazini, zinazounganisha Vijiji ambazo hazipitiki kwa sasa?”

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Tamisemi, David Silinde amesema, Singida Kaskazini ina mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 811.68 ambao umekuwa ukifanyiwa matengenezo pamoja, kujenga na kukarabati vivuko.

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

“Katika mwaka wa fedha 2019/20, Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (Tarura), Halmashauri ya Wilaya ya Singida, ilifanya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 78.55 na vivuko 22 kwa gharama ya Sh.739.39 milioni.”

“Katika mwaka fedha 2020/21, barabara zenye urefu wa kilomita 67.8 na vivuko 20 vimetengenezwa kwa gharama ya Sh. 711.08 Milioni ambapo hadi Machi 2021 barabara zenye urefu wa kilomita 45 na vivuko 15 vimekamilika,” ameeleza Silinde.

Pia, katika mwaka wa fedha 2021/22 barabara zenye urefu wa kilomita 62.5 na vivuko 24 vitajengwa kwa gharama ya Sh. 711.08 Milioni

“Serikali kupitia Tarura, halmashauri ya wilaya ya Singida, itafanya tathmini ya barabara zote za Singida Kaskazini ili kuandaa mpango wa namna bora ya kuweka vipaumbele vya ujenzi na matengenezo ya barabara,” amesema Silinde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!