Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mbunge adakwa akitazama video za ngono bungeni
KimataifaTangulizi

Mbunge adakwa akitazama video za ngono bungeni

Spread the love

CHAMA cha Conservative kutoka nchini Uingereza kimemsimamisha uanachama Mbunge wa Jimbo la Tiverton na Honiton, Neil Parish baada ya kubambwa akitazama video za ngono akiwa bungeni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mbunge huyo (65) kutoka chama cha Conservative amekumbwa na mkasa huo mzito baada ya wabunge wenzake wawili wa kike kutoa ushuhuda kuwa walimuona akitazama video hizo chafu kwa nyakati tofauti.

Jana tarehe 29 Aprili, 2022 wabunge hao wamesema walimuona Parish akiangalia video hizo chafu akiwa bungeni na kwa mara ya pili alikuwa katika vikao vya kamati.

Aidha, kutokana na kashfa hiyo mbunge huyo aliyedumu bungeni kwa zaidi ya miaka 12, amekiri kufungua ‘file’ la video hizo kwa bahati mbaya.

Pia amejitetea kwamba atakuwa tayari kutoa ushirikiano wote kwa wahusika wa uchunguzi wa sakata hilo.

Hata hivyo, mke wa mbunge huyo amemtetea mumewe na kudai kuwa ni mtu mwema na hajawahi kuwa na tabia hiyo katika kipindi cha miaka 40 ya ndoa yao.

Aidha, amesisitiza kuwa watu hawatakiwi kuangalia video za ngono kwani ni udharirishaji kwa wanawake.

Kutokana na mkasa huo, kumekuwa na shinikizo kutoka kwa wabunge wenzake wakimtaka Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson kumuwajibisha kwa kumuondoa madarakani.

Wabunge wengine hasa wa kike akiwemo Harriet Harman Kutoka chama cha Labour amemtaka ajiuzulu wadhifa wake kwani hafai kuwa mbunge na haoneshi picha nzuri kwa jamii.

Naye Waziri Rachel Maclean amepigilia msumari kuwa mbunge huyo anatakiwa kujiuzulu mara moja.

1 Comment

  • Halafu hawa ndio wanatufundisha demokrasia na utawala bora. Unafiki tu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!