Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, wabunge Chadema ‘waliamsha dude’ ofisi za Tume
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, wabunge Chadema ‘waliamsha dude’ ofisi za Tume

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema (katikati) akiwa na Mgombea Ubunge Kinondoni, Salum Mwalimu walipowasili ofisi za NEC
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiongozana na Mgombea Ubunge Jimbo la Kinodnoni, Salumu Mwalimu pamoja na wabunge wa Chadema katika ofisi za Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhoji sababu za mawakala wake kutopewa hati za viapo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbowe akiongozana na wenzake amelazimika kufika katika ofisi hizo kwa lengo la kuhoji sababu zilizofanya mawakala wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni wasipewa nakala za viapo hadi leo huku ikiwa uchaguzi unatarajiwa kufanyika Februari 17, mwaka huu.

Mwenyekiti huyo pamoja na kuongozana na Mwalimu, mgombea ubunge wa jimbo hilo, pia ameongozana na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini na mwanachama wengine wa chama hicho.

“Tumekuja Tume kuonana na Mkurugenzi wa Tume Taifa juu ya hujuma zinazofanywa na Mkurugenzi wa Kinondoni kwa kutowapa mawakala wetu nakala za kiapo mpaka sasa hivi,” amesema Mbowe.

Lakini pamoja na Mbowe na wenzake kufika ofisini hapo, wameambiwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhani Kailima hayupo ofisini na wameahidi kuendelea kubaki mpaka atakaporudi ofisini.

MwanaHALISI Online itaendelea kuwapa taarifa nini kinachopendelea katika ofisi za NEC.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

error: Content is protected !!