Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Najivika mabomu kumpongeza Samia “angeendeleza kiburi cha mtangulizi wake”
Habari za Siasa

Mbowe: Najivika mabomu kumpongeza Samia “angeendeleza kiburi cha mtangulizi wake”

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe amesema anatambua kuwa ni vigumu kuwaeleza Watanzania na dunia kwamba anampongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali maridhiano ya kitaifa ila anajivika mabomu kufanya hivyo kutokana na hatua njema iliyofikiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Amesema angeweza kuendeleza kiburi cha mtangulizi wake lakini kutokana na ushawishi wake na wanachadema na viongozi wa CCM wenye busara wamefikia pazuri.

Mbowe ametoa kauli hiyo leo tarehe 21 Januari, 2023 wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza katika uzinduzi rasmi wa mikutano ya hadhara.

Amesema hakuna nchi duniani ambayo imeshawahi kujengwa kwa demokrasia dhoofu kwani demokrasia ikikua na uchumi utakua.

Aidha, amemuomba Rais Samia asikwazike pale ambapo Chadema watampinga kwa nguvu zote katika baadhi ya ajenda.

“Nchi yetu inahitaji Katiba bora, usidanganywe na yeyote kuondoka bila katiba bora, lazima kuwepo na katiba bora ili tusirudi tena kwenye zile chaguzi za kihuni… za watu wanaiba uchaguzi na kuwa huru mitaani.

“Yeyote anayeiba lazima awajibishwe, pale ambapo tunaamini sheria zitasimama kwenye haki wanaostahili, hazitamkandamiza yeyote ili kwa pamoja tulijenge Taifa salama, linaloitengeneza kesho ya watoto wetu kuwa kesho bora zaidi.

“Tutaendelea kuzungumza na ushirikiano lakini tukiwa makini kuliko makini yenyewe.Tutapiga jaramba mpaka kieleweke!” amesema Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!