Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe na wenzake wakamilisha dhamana, waachiwa huru
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe na wenzake wakamilisha dhamana, waachiwa huru

Viongozi wa Chadema wakiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wenzake sita akiwemo Halima Mdee, Mbunge wa Kawe aliyeunganishwa katika kesi hiyo leo, wamekamilisha masharti ya dhamana hivyo wakati wowote wanaweza kuachiwa huru. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imejiridhisha na nyaraka walizoziwasilisha wadhamini kwa ajili ya dhamana ya washtakiwa hao na imewakubalia kuwadhamini huku ikiwapa maelekezo kuhakikisha kuwa wanapatikana mahakamani kila wanapohitajika.

Masharti ya dhamana yao ni kusaini bondi ya Sh 20 milioni  kuwa na wadhamini wawili wenye barua kutoka ofisi za Serikali za mitaa au vijiji na kuripoti kituo kikuu cha Polisi kila Alhamisi.

Mbali ya Mbowe wengine ni Katibu Mkuu Dk Vicent Mashinji, manaibu katibu wakuu John Mnyika (Bara), Salum Mwalimu (Zanzibar), Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa na Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake wa chama hicho, Ester Matiko  na Mwenyekiti wake, Halima Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe, wanaokabiliwa na kesi ya jinai, wakidaiwa pamoja na mambo mengine ikiwamo kufanya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali.

Kabla ya Mdee kupata dhamana pamoja na wenzake mawakili wa Serikali wapinga mahakama kumpa dhamana Mdee kwa sababu kabla hajafikishwa mahakamani alipewa dhamana Polisi lakini hakukidhi masharti kwa kushindwa kuripoti polisi wasema wanahofu akipewa dhamana ya mahakama hataweza kutimiza wajibu wake.

Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri hakukubaliana na madai ya mawakili wa Serikali kwani Mahakama haiwezi kumnyima mshtakiwa dhamana kwa sababu aliruka dhamana ya polisi kwa kuwa hizo ni taasisi mbili tofauti na haziwezi kuingiliana.

Kesi hiyo itatajwa tena Aprili 16, 2018. Watuhumiwa hao walikuwa mahabusu tangu walipopandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo Machi 27 mwaka huu, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!