VIONGOZI tisa wa Chama cha Demokrasia na Maanedeleo (Chadema), wanatarajiwa kutinga mahakamani tena kesho kusikiliza kesi inayowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Wanaotarajiwa kufika mahakamani kesho, ni pamoja na Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa chama hicho; Dk. Vicenti Mashinji, katibu mkuu; John Mnyika, naibu katibu mkuu na Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake taifa (BAWACHA).
Wengine, ni Salum Mwalimu, naibu katibu mkuu Zanzibar; Esther Matiko, mbunge wa Tarime Mjini; Mchungaji Peter Msigwa, mbunge wa Iringa Mjini; Ester Bulaya na John Heche, mbunge wa Tarime Vijijini.
Viongozi hao wandamizi wa chama hicho ambacho ni kikuu cha upinzani nchini, wanatuhumiwa kwa makosa mbalimbali, ikiwamo kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali na uchochezi.
Mbele ya Hakim Mkuu Mkazi Mashauri, watuhumiwa wote wanadaiwa kutenda tendo hilo, tarehe 26 Februari mwaka huu.
Wamekana madai hayo.
Leave a comment