Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe na wenzake mahakamani tena kesho
Habari za Siasa

Mbowe na wenzake mahakamani tena kesho

Viongozi wa Chadema wakiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

VIONGOZI tisa wa Chama cha Demokrasia na Maanedeleo (Chadema), wanatarajiwa kutinga mahakamani tena kesho kusikiliza kesi inayowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wanaotarajiwa kufika mahakamani kesho, ni pamoja na Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa chama hicho; Dk. Vicenti Mashinji, katibu mkuu; John Mnyika, naibu katibu mkuu na Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake taifa (BAWACHA).

Wengine, ni Salum Mwalimu, naibu katibu mkuu Zanzibar; Esther Matiko, mbunge wa Tarime Mjini; Mchungaji Peter Msigwa, mbunge wa Iringa Mjini; Ester Bulaya na John Heche, mbunge wa Tarime Vijijini.

Viongozi hao wandamizi wa chama hicho ambacho ni kikuu cha upinzani nchini, wanatuhumiwa kwa makosa mbalimbali, ikiwamo kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali na uchochezi.

Mbele ya Hakim Mkuu Mkazi Mashauri, watuhumiwa wote wanadaiwa kutenda tendo hilo, tarehe 26 Februari mwaka huu.

Wamekana madai hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!