Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Mbatia ‘bifu’ kali
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Mbatia ‘bifu’ kali

Spread the love

JAMES Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amekataa kufanya kazi na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Kutokana na hali hiyo, Mbowe amelazimika kuunda baraza jipya la mawaziri kivuli leo tarehe 3 Aprili 2020.

“Nilimuuliza (Mbatia) kama yupo tayari kufanya kazi kwani nilimweleza nataka kuufanya mabadiliko, alisema atafurahi kama nitamuacha,” amesema Mbowe.

Mbatia amekuwa akisakamwa na makada wa Chadema kwamba, anatumika kukibomoa chama hicho. Ni baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli Ikulu, jijini Dar es Salaam. Mara kadhaa Mbatia amekuwa akipinga tuhuma hizo.

Mbatia alikutana na Rais Magfuli kama ambavyo viongozi wengine wa vyama vya upinzani akiwemo Maalim Seif Sharif Hamadi, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo na Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) walivyokutana naye.

Kwenye baraza hilo jipya, Mbowe amewaondoa wabunge wote wanaotokana na vyama vingine na kubakisha wale wa Chadema pekee huku akieleza ‘mazingira ya siasa yamebadilika.’

Akizungumzia kuwaacha wabunge wa CUF, Mbowe amesema, uamuzi huo ni baada ya Maalim Seif kuhamia ACT-Wazalendo.

Amesema, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haikuwa ikifanya kazi na Kambi ya Prof. Lipumba, hivyo kwa kuwa Maalim Seif aliondoka CUF, hakuona sababu ya kuendelea kukihusisha chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!