MALI za kampuni ya Mbowe Limited, inayomilikiwa na mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, zimapangwa kupigwa mnada, Jumamosi wiki hii. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na kampuni ya udalali ya Fosters Auctionare ya jijini Dar es Salaam, kufanyika kwa mnada huo, kunatokana na Mbowe kushindwa kulipa deni la Sh. 1.1 bilioni, anazodaiwa na Shirika la Nyumba la taifa (NHC).
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo ya udalali, Joshua Mwaituka, amemueleza mwandishi wa MwanaHALISI ONLINE, mnada huo utafanyika kwenye ghala la NHC lililopo karibu na geti Na. 3, eneo la bandarini jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 4 asubuhi.
Mwakituka ametaja baadhi mali zitakazopigwa manada, kuwa ni pamoja na taa, makabati, meza, makochi, viti na vitu vingine, majukwaa na vifaa vingine vilivyokuwa vikitumika kwenye ukumbi huo.
“Tumeelekezwa na NHC, kupiga mnada mali za kampuni ya Mbowe Limited, kufuatia wamiliki wake, kushindwa kulipa kodi kwa miaka 20. Thamani ya deni wanalodaiwa, ni Sh. 1.1 bilioni,” ameeleza Mwakituka.
Alipoulizwa kama wanadhani vitu wanavyouza, vitaweza kutosha deni wanalodai au wanafanya hivyo kwa misingi ya kisiasa, Mwakituka amesema, “tunauza kwa maelekezo ya mteja wetu NHC. Kama fedha itatosha au haitatosha, hilo tutalijua baadaye.”
Mbali na vitu ambavyo vilikuwa vinatumika kwenye ukumbi wa disco wa Bilicanas, vitu vingine vitakavyopigwa mnada, ni komputa, meza, makabati na viti, ambavyo vilikuwa vinatumiwa na kampuni ya Free Media, iliyokuwa inamiliki gazeti la Tanzania Daima.
Leave a comment