Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe awaachia kibarua Watanzania 28 Oktoba
Habari za Siasa

Mbowe awaachia kibarua Watanzania 28 Oktoba

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewaomba Watanzania kuutumia Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020, kuamua mustakabali mwema wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Mbowe ametoa ombi hilo jana Jumatatu tarehe 19 Oktoba 2020, wakati akimuombea kura Mgombea Urais wa Tanzania wa Chadema, Tundu Lissu kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Moshi Mjini mkoa wa Kilimanjaro.

Mwenyekiti huyo wa Chadema ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Hai, aliwaomba Watanzania, watafakari nchi yao ilipotoka, iliko na inakoelekea ili kuutumia uchaguzi huo kurekebisha makosa yaliyojitokeza.

“Watanzania wote, nahitaji kila mwananchi aungane na mamilioni ya Watanzania wengine kuitafakari nchi hii imetoka wapi, iko wapi na inaenda wapi.  Tumeona matendo ya kikatili sana, tunataka wananchi wawe huru,” alisema  Mbowe

“Kwa sasa, wanaumzwa wafanyabiashara, Tunawaambia wana siku nane, baada ya siku nane masuala kama haya lazima Watanzania  tuyamalize kwa kumpigia kura za kishindo Tundu Lissu, wagombea udiwani na ubungo,” alisema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!