Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe atoa msimamo makongamano ya Katiba
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe atoa msimamo makongamano ya Katiba

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

FREEMAN Mbowe amesema, watafanya kongamano la Katiba jijini Mwanza keshokutwa Jumatano, tarehe 21 Julai 2021 na mikoa mingine yataendelea “hadi Katiba mpya itakapopatikana.”. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ni baada ya kutofanyika kwa kongamano hilo juzi Jumamosi na kujikuta baadhi ya wanachama na viongozi wa chama hicho zaidi ya 38 wakitiwa nguvuni na Jeshi la Polisi.

Kati ya waliokamatwa ni Askofu wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Emmaus Mwamakula na Mhadhiri Mwandamizi wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azaveli Lwaitama ambao wasisota rumande hadi jana jioni Jumapili, walipoachiwa.

Mara baada ya kutofanyika kwa kongamano hilo kwa madai ambayo polisi wamesema hawakuwa na taarifa, Mbowe aliyekuwa katika maombolezo ya msiba wa kaka yake, Charles, mkoani Kilimanjaro, alisitisha na kwenda Mwanza.

DK. Azaveli Lwaitama, Mhadhiri mstaafu

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo Jumatatu, tarehe 19 Julai 2021, makongamano ya Katiba yataendelea kufanyika nchi nzima hadi siku itakayopatika katiba mpya.

“Hatutaondoka hapa Mwanza na wiki hii tufanya kongamano kubwa hapa Mwanza, sisi viongozi hatutaondoka Mwanza na kama polisi wanataka kutukamata basi waanze kunikamata mimi Mbowe,” amesema Mbowe

Katika kusisitiza hilo amesema “tutafanya makongamano haya nchi nzima hadi tupate katiba mpya kwani Katiba ya nchi ni katiba ya Taifa, haipaswi kuwa Katiba ya chama na haipaswi kuwa na kiongozi yoyote atakayezuia mjadala wa Katiba.”

Mbowe amesema, harakati za kudai katiba mpya si ya chama cha siasa peke yake “na ili polisi wasituondoe kwenye mstari, kwa sasa mwanachama wetu akiwekwa ndani, hatutamwekea dhamana. Kwani mikutano hii tunaifanya kwa mujibu wa Katiba na sheria.”

2 Comments

  • Asante mwenye kiti kwa maelezo yako lakini uwelewe kufuata sheria ni lazima na walala sio jambo laiyairi sheria ukivunja sheria mkono wa sheria utakufunza sheria .pia uwelewe ndugu mbowe wananchi hawana tazizo na katiba yasasa wananchi wanaitaji mafaniko yenye maendeleo na ccm imewaidi wananchi kuwa itatimiza mahitaji yote muhmu kwa wananchi ccm haikusema nichagueni mpate katiba mpya ccm imetamka tuchagueni mpate mabadiliko yenye manufa kwa nchi na wananchi sasa ndugu mbowe swala lako katiba mpya ni sawa na kumpigia gita mbuzi

  • Ndugu S,
    Maendeleo hayatokani na chama chochote, bali yanatokana mipango ya maendeleo inayoratibiwa na wataalamu (technocrats).
    Ilituchukua miaka 30 ya upotevu hadi hayati Magufuli aliposimamia maendeleo ya kimkakati.
    Wapinzani wangeongoza miaka 10 tu kati ya hiyo 30 tungefika mbali sana!
    Waulize wamexico!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!