Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe anena mazito wakili wao kujitoa
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe anena mazito wakili wao kujitoa

Spread the love

BAADA ya Jeremiah Mtobesya, wakili anayetetea viongozi waandamizi wa Chadema wanaokabiliwa na kesi ya jinai namba 112, kujitoa katika kesi hiyo. Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho Taifa ameendelea kuonyesha kutoridhishwa kwake na uendeshaji wa Hakimu Wilbard Mashauri. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 23 Agosti, 2018, Mbowe amesema kitendo cha wakili huyo kujitoa katika kuwatetea kinadhihirisha kile alichokiita kuwa, Hakimu Mashauri anaendesha kesi yao kwa kufuata maagizo yaliyotoka juu badala ya kufuata sheria.

Mbowe ameeleza kuwa, malalamiko yao kuhusu kutokuwa na imani na Hakimu Mashauri hayamaanishi kama wanaogopa kufungwa, bali hawataki kufungwa kwa makosa wasiyokuwa na hatia nayo.

Mbowe amedai kuwa, Hakimu Mashauri anaiendesha kesi hiyo haraka haraka kana kwamba anapokea mashinikizo kutoka juu.

“Tuliwahi kufikia hatua ya kumkataa hakimu kutokana na mwenendo wake unaonyesha kama anaendesha kesi kwa mashinikizo. Hatua hii imechosha mawakili wetu. Wakili amejitoa bado hakimu akataka kesi kesho iendelee,” amesema.

Wakili Mtobesya alijitoa katika kesi hiyo baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuyatupilia mbali maombi ya washtakiwa ya kutaka kesi hiyo iahirishwe. Ili kusubiri maombi yao ya rufaa yaliyopo katika mahakama ya rufani.

Viongozi hao wa Chadema wapatao tisa wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwemo ya kufanya mkusanyiko kinyume na sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!