Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mbinu za China zaishtua FBI
Kimataifa

Mbinu za China zaishtua FBI

Spread the love

CHRISTOPHER Wray, Mkurugenzi wa Shirika la Upelelezi la Mareani (FBI) amesema, vitendo vya Serikali ya China ni tishio kwa taifa hilo. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Akizungumza katika Taasisi ya Hudson ya mjini Washington, Wray amesema China inaendesha upelelezi na wizi jambo ambalo ni tishio kubwa la Marekani katika siku za mbele.

”China imeanza juhudi za kuhakikisha kuwa ndio taifa la pekee litakalokuwa na uwezo mkubwa zaidi duniani kwa hali na mali,” aliongezea.

Mkurugenzi huyo amesema, China imekuwa ikiingilia masuala mbalimbali ya Marekani kupitia kampeni kubwa ya upelelezi wa uchumi wa Marekani, wizi wa data na fedha.

”Tumefikia wakati ambapo FBI sasa imeanza kufungua kitengo cha kukabiliana na visa vya Ujasusi wa China kila baada ya saa 10. Kati ya visa 5000 vya kukabiliana na ujasusi vinavyoendelea kote nchini, karibia nusu yake vinahusishwa na China,” amesema.

Rais wa China, Xi Jinping (kulia) akisalimiana na Donald Trump, Rais wa Marekani

Amemtuhumu Rais wa China, Xi Jinping kwamba ameanzisha mpango kwa jina ‘Fox Hunt’, unaowalenga raia wa China ughaibuni wanaoonekana kuwa tishio kwa Serikali ya China.

”Tunazungumzia kuhusu wapinzani wa kisiasa, watoro na wakosoaji walio na lengo la kufichua ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na China,” amesema na kuongeza:

”Serikali ya China inataka kuwalazimisha kurudi nyumbani na mbinu zinazotumiwa na China kufanikisha mpango huo inashtua. Inaposhindwa kumpata mtu inayemtafuta, serikali ya China hutuma mjumbe kutembelea familia ya mtu huyo nchini Marekani. Ujumbe unaotolewa ni ‘Rudi China haraka ama jiue.’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!