Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia, wenzake wakwaa kigingi, Mahakama yawatambua wajumbe wapya wa bodi
Habari za Siasa

Mbatia, wenzake wakwaa kigingi, Mahakama yawatambua wajumbe wapya wa bodi

Joseph Selasini (kulia) na James Mbatia
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu, Masjala Kuu ya Dar es Salaam, imetoa uamuzi wa kuwatambua wajumbe wapya wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha NCCR-Mageuzi, hadi kesi ya msingi iliyofunguliwa na wajumbe wa zamani kupinga uhalali wa vikao vilivyowateua itakapotolewa uamuzi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Uamuzi huo umetolewa na mahakama hiyo jana tarehe 6 Februari 2023, mbele ya Jaji Ephery Kisanya, wakati kesi hiyo ndogo Na. 570/2023, ilipokuja kwa ajili ya kutolewa uamuzi.

Jaji Kisanya alitoa uamuzi huo akisema, kama mahakama hiyo ingetoa uamuzi kuhusu uhalali wa vikao vilivyofanya uteuzi wao, ingeathiri kesi ya msingi ambayo bado haijatolewa uamuzi.

Amesema kuwa, mahakama hiyo imeamua kuwatambua wajumbe hao ambao ni Beati Mpitabakama, Ester Komba, Laila Rajab Hamis, Mtumwa Ame Hamis na Idrisa Omary Haji, kulingana na ushahidi ulioletwa mahakamani hapo na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), uliowatambua kuwa ni wajumbe halali.

Kesi hiyo ndogo ilifunguliwa na wajumbe wa zamani, Mohamed Tibanyendera na wenzake, dhidi ya Joseph Selasini na wenzake, wakiwatuhumu kuwaondoa katika nyadhifa zao kinyume cha sheria, kisha kujiteua katika nafasi hizo.

Katika kesi hiyo, Tibanyendera na wenzake walidai kikao kilichotumika kuwaondoa ujumbe tarehe 23 Mei 2022 hakikuwa halali.

Baada ya mahakama kutoa uamuzi huo, Jaji Kisanya ameahirisha kesi ya msingi hadi tarehe 14 February 2023, itakapokuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Katika kesi ya msingi Na. 150/2022, Tibanyendera na wenzake wanapinga kufukuzwa NCCR-Mageuzi wakidai kwamba mkutano uliotoa maamuzi hayo tarehe 21 Mei 2022 haukuwa halali kwa kuwa uliahirishwa na uongozi wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wake anayedaiwa kufukuzwa, James Mbatia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!