JESHI la polisi mkoa wa Morogoro linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kumkata mkono mlemavu wa ngozi /albino katika kijiji cha Nyarutanga kata ya Kisaki wilaya ya Morogoro Vijijini, anaandika Christina Haule.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro (ASP) Leonce Rwegasira, amesema kuwa tukio la kwanza lilitokea Oktoba 3 saa 6 usiku katika kijiji cha Nyarutanga ambapo watu wasiojulikana walivamia nyumba ya Nassoro Msingili (75) mkazi wa kijiji ambaye ni mlemavu wa ngozi/albino na kumkata mkono wa kushoto.
Kamanda huyo amesema kuwa Msingili akiwa amelala ndani ya nyumba yake alivamiwa na watu hao wasiojulikana na kisha kumkata mkono wake wa kushoto na kukimbia nao kusikojulikana.
Amesema majeruhi huyo amelazwa katika kituo cha afya Duthumi akiendelea kupatiwa maibabu huku yake ikizidi kuimarika.
Hata hivyo amesema juhudi za kuwatafuta waliofanya uhalifu huo zinaendelea ambapo tayari watu wawili ambao hakutaja majina yao kufuatia kuendelea kufanya uchunguzi ili kubaini watu wote waliohusika katika tukio hilo.
Aidha amesema jeshi hilo linapinga vikali mauaji na ukatili unaofanywa kwa albino na linaendeleza msako mkali kuwasaka wale wote wanaojihusisha na matukio kama hayo.
Leave a comment