Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Hatma ya Mbao FC, Mbeya City Ligi Kuu leo
Michezo

Hatma ya Mbao FC, Mbeya City Ligi Kuu leo

Mbeya City
Spread the love

KLABU za Mbao FC pamoja na Mbeya City zinashuka dimbani leo katika michezo ya marudiano ya mtoano (Play off) katika harakati za kuwania kusalia Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu ujao wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Michezo ya mzunguko wa kwanza Mbao FC ilipoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya Ihefu kutoka Mbeya, huku Mbeya City ikilazimshwa sare ya bao 1-1 na Geita Gold kutoka Shinyanga.

Katika michezo Mbao FC itakuwa nyumbani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba dhidi ya Ihefu huku ikiitaji ushindi wa mabao matatu ili iweze kusalia kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu ujao.

Wachezaji wa Mbao FC

Kwa upande wa Mbeya City nao watakuwa nyumbani kwenye Uwanja wa Sokoine kujiuliza mbele ya Geita Gold kwa kuhitaji sare ya bila kufungana au kupata ushindi wowote ili iweze kusalia kwenye Ligi Kuu kwa msimu ujao.

Ligi Kuu Tanzania Bara tayari imeshamalizika wiki iliyopita huku klabu za Alliance, Ndanda FC, Lipuli FC na Singida United zikishuka daraja huku klabu za Gwambina na Dodoma United zikipanda Ligi Kuu kwa msimu ujao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!