ZAIDI ya watu 30, wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa katika msongamano wa watu, waliojitokeza kumzika Qasem Soleiman, aliyekuwa kiongozi mwandamizi wa Jeshi la Irani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, tukio hilo limetokea leo tarehe 7 Januari 2020 katika Mji wa Kerman, kufuatia msongamano mkubwa wa mamilioni ya watu, waliojitokeza kumzika Jenerali Soleiman, aliyefariki dunia tarehe 3 Januari 2020, nchini Iraqi.
Jenerali Soleiman aliuawa katika shambulio la anga, lililotekelezwa na Nchi ya Marekani, mjini Baghdad nchini Iraqi.
Leave a comment