Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari Mazishi ya Magufuli: Dk. Shein akumbusha machungu uchaguzi mkuu 2015
Habari

Mazishi ya Magufuli: Dk. Shein akumbusha machungu uchaguzi mkuu 2015

Aliyekuwa rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Spread the love

 

RAIS Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein amesema, aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli (61), alikuwa mshauri wake katika mgogoro wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato…(endelea).

Dk. Shein amesema hayo leo Ijumaa tarehe 26 Machi 2021, mara baada ya kumalizika kwa misa takatibu ya mazishi ya Dk. Magufuli, iliyofanyika uwanja wa mpira wa miguu wa Magufuli, wilayani Chato Mkoa wa Geita.

Dk. Magufuli amefariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya ugonjwa wa mfumo wa umeme wa moyo. Mwili wake unazikwa leo nyumbani kwao Chato.

“Dk. Magufuli nilikuwa namuamini sana, katika muungano alinitia moyo sana, hasa baada ya matukio yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu. Kaniambia bwana wee chapa kazi watu wataona wenywe,” amesema Dk. Shein.

Rais huyo mstaafu wa Zanzibar amesema, katika enzi za uhai wake, Dk. Magufuli hakuwahi kumshauri vibaya.

“Nimejitahidi kufanya hivyo kufuata mfano wake, kufuata ushauri wake na hakunishauri vibaya hata siku moja,” amesema Dk. Shein.

Katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, kuliibuka mgogoro baina ya Dk. Shein na aliyekuwa mpinzani wake wa karibu katika kinyang’anyiro cha kiti cha urais wa Zanzibar, Hayati Maalim Seif Shariff Hamad, baada ya matokeo ya uchaguzi huo kufutwa.

Katika uchaguzi huo, Dk. Shein aligombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku Maalim Seif aliyefariki dunia tarehe 17 Februari 2021, alikuwa mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF).

Uchaguzi huo ulifutwa na Jecha Salim Jecha, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kwa maelezo kwamba mchakato wake ulikuwa na dosari. Kisha akaitisha uchaguzi wa marudio, ambao Maalim Seif alisusa kushiriki.

Baada ya uchaguzi huo wa marudi kuitishwa, Dk. Shein alishinda uchaguzi huo, na kuunda Serikali huku CUF wakisusia kushiriki uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!