Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawakili waiburuza mahakamani TLS, EALS
Habari Mchanganyiko

Mawakili waiburuza mahakamani TLS, EALS

Wakili Hekima Mwasipu
Spread the love

 

WAKILI Hekima Mwasipu na wenzake wawili, wamefungua kesi katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu, jijini Dar es Salaam, kupinga masharti mapya yanayowalazimisha mawakili kuwa wanachama wa Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Leo tarehe 8 Februari 2023, kesi hiyo Na. 2/2023, kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa mahakamani hapo, mbele ya Jaji Moses Mzuna.

Jaji Mzuna alitoa amri kwa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika na EALS, ambao ni washtakiwa katika kesi hiyo pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kuwasilisha hati kinzani ndani ya siku 14 kuanzia leo, hadi tarehe 28 Februari 2023.

Baada ya kutoa amri hiyo, Jaji Mzuna aliahirisha kesi hiyo hadi tarehe 1 Machi mwaka huu, ambapo itakuja kutajwa tena.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kesi hiyo kuahirishwa, Wakili wa waleta maombi, Selemani Matauka, amedai wateja wake wamefungua kesi hiyo kupinga sharti la wanachama wote wa TLS kuwa wanachama wa lazima wa EALS, ilhali taasisi hiyo ni kampuni binafsi.

Pia, wanapinga kipengele cha kutopewa vitambulisho vya uwakili vya uanachama wa TLS, hadi watakapolipa ada ya uanachama wa EALS, kiasi cha Dola za Marekani 20.

Mbali na Wakili Mwasipu, mawakili wengine waliofungua kesi hiyo ni, Frank Chundu na Deogratius Mahinyira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!