Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mawakala Chadema, NCCR wasulubiwa Ukonga
Habari za Siasa

Mawakala Chadema, NCCR wasulubiwa Ukonga

Spread the love

MSIMAMIZI wa kituo cha Uchaguzi Pugu mnadani, Mustapha Zayumba amewatimua mawakala Chadema, NCCR-Mageuzi na NLD. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mustapha amesema, amewatimua mawakala hao kwa madai ya kutokuwa na barua za mtendaji wa kata.

Mawakala wa Chadema wamelalamika kwamba, katika viapo waliyopewa vya kusimamia uchaguzi, walielezwa kuwa fomu zote watazikuta kituoni.

“Nashangaa eti hapa wanatuambia haturuhusiwi kusimamia mpaka tuwe na viapo na barua za mtendaji jambo ambalo awali hawakueleza mahitaji hayo,” alilalamika wakala mmoja na kuongeza:

“Tumekwenda kwa mtendaji hatujamkuta hivyo tunaonekana hatuna sifa.”

Msimamizi Mustapha amesema, hata mawakala wa CCM nao walitimuliwa na kwamba, wamekwenda kufuata barua hizo.

Amesema “hakuna wakala yoyote anayependelewa ila utaratibu lazima ufuatwe.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!