Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mauzo ya figo yaongezeka mtandaoni
Kimataifa

Mauzo ya figo yaongezeka mtandaoni

Spread the love

 

HOSPITALI kuu ya umma kutoka nchini Kenya, imeripoti kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la idadi ya watu wanaoulizia nakujitolea kuuza figo zao. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea)

Katika chapisho la Facebook kutoka Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, imetipoti kuwa ‘’Figo yangu ni pesa ngapi?’’ hilo ni swali lililoulizwa zaidi kupitia ujumbe kwenye ukurasa wao.

Hata hivyo hospitali hiyo ilishauri kwamba viungo vya mwili vinaweza kutolewa kwa wagonjwa tuna kusisitiza kuwa “tafadhali kumbuka uuzaji wa viungo ni marufuku na ni kinyume cha sheria, unaweza kuchangia kwa hiari yako,” ilisema.

Bango la hospitali hiyo, linaangazia hatua za kukata tamaa ambazo watu wanafikiria huku kukiwa na ongezeko la bei ya chakula na mafuta.

Aidha benki ya dunia, mapema mwezi huu imeonya kuwa Afrika mashariki ni miongono mwa maeneo yanayokabiliwa na mdororo mkubwa wa uchumi kwa sababu ya vita vya Urusi nchini Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!