Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maumivu mapya 17 ya tozo
Habari MchanganyikoTangulizi

Maumivu mapya 17 ya tozo

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

WAKATI wananchi wakiendelea kuugulia juu ya tozo za miamala ya simu, majengo na mafuta, Serikali inakuja na maumivu mengine ya tozo 17 za kazi mbalimbali za wasanii. Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Baadhi ya maeneo yanayopendekezwa ni kwenye; vituo vya redio, televisheni, vituo vya kuuza mafuta vyenye vifaa vya muziki, maduka ya madawa ya binadamu, benki na taasisi nyingine za kifedha pamoja na maeneo ya kufanyia mazoezi ‘gym.’

Pia, maeneo yanayopiga karaoke, maonyesho kwa umma kwenye vyumba vya hoteli, viwanja vya ndege za ndani na za kimataifa, vyombo vya usafiri, maonyesho kwa umma katika mabaa, pubs, klabu na grosari na maonyesho kwa umma kwa kazi za filamu.

Maandalizi ya tozo hizo ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyeagiza wizara ya habari, utamaduni, saana na michezo kuhakikisha ifikapo Desemba 2021, wasanii wanaanza kulipwa mirabaha.

Rais Samia alitoa maagizo hayo tarehe 15 Juni 2021, wakati akizungumza na vijana jijini Mwanza akisema “kuanzia Desemba 2021, wasanii wataanza kulipwa mirabaha kwa kazi zao zinazotumiwa katika radio, televisheni au mitandaoni.”

Tayari Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) imeandaa kanuni ya leseni na haki ya kuuzwa tena kwa kazi za ubunifu zikiwa na viwango vya mapendekezo ya ada pamoja na sababu za kuanzishwa kwa tozo hizo.

Endapo mapendekezo hayo yatapitishwa na kuanza kutumika, utakuwa mzigo mwingine kwa wananchi ambao haohao wanaendelea kukamuliwa kwenye tozo za miamala ya simu, mafuta na majengo.

Undani wa habari hii na viwango vinavyopendekezwa kwa kina eneo, soma gazeti la Raia Mwema toleo la leo Jumamosi tarehe 21 Agosti 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!