Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Matenki ya mafuta kujengwa Tanga
Habari Mchanganyiko

Matenki ya mafuta kujengwa Tanga

Matanki ya GBP yaliyopo mkoani Tanga
Spread the love

KAMPUNI ya mafuta ya GBP imepanga kutumia zaidi ya 60 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa bohari ya kuhifadhia mafuta na kiwanda cha gesi ili kuongeza huduma na kupunguza kero ya upatikanaji wa bidhaa hizo, anaandika Mwandishi Wetu.

Mkurugenzi wa GBP, Badar Sood alieleza kuwa kampuni hiyo ina mpango wa kujenga matenki zaidi yenye uwezo wa kuhifadhi lita 300 na kwamba bohari ya sasa inahifadhi lita million 122.6.

Sood amesema sambamba na ujenzi wa matanki hayo ambayo mradi wake umezinduliwa juzi na Rais John Magufuli, utaambatana na mpango wa kujengwa kwa kiwanda cha gesi ambavyo vyote kwa pamoja vinatarajiwa kugharimu jumla ya Sh. 60 bilioni.

“Ujenzi wa matenki hayo umepunguza foleni ya malori jijini Dar es Salaam pamoja na uharibifu wa barabara” ameeleza Sood.

Ameeleza ya kampuni hiyo kuwa pamoja na mambo mengine ni kufanya uwekezaji mkubwa kwa kutumia meli kubwa na hivyo kupunguza gharama za usafirishaji wa bidhaa hiyo.

Katika kusaidia jamii, Mkurugenzi huyo ameleza kuwa uwekezaji wake umejikita katika ushiriki wa harakati za maendeleo ikiwemo kuchangia sekta ya elimu kwa kutoa jumla ya mifuko 2000 ya saruji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!